Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 140 2022-11-11

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutoa mwongozo wa upandishaji mishahara kwa wafanyakazi wa sekta binafsi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mshahara katika sekta binafsi unapanda baada ya Bodi ya Kima cha Chini cha Mishahara katika sekta binafsi ambayo inaundwa kwa mujibu wa Sheria ya Taasisi za Kazi, Sura ya 300 kufanya utafiti na kupanga viwango vya mishahara katika sekta binafsi.

Mheshimiwa Spika, ninapenda kulijulisha Bunge lako tukufu kuwa Bodi hiyo tayari imekamilisha kazi ya kupanga kima cha chini kipya na kumshauri Waziri mwenye dhamana na masuala ya kazi ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi. Kwa ujumla, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha suala hili na itatangaza rasmi kima cha chini cha mshahara katika sekta binafsi mwezi huu wa Novemba, 2022. Ahsante.