Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 85 2022-11-07

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI K.n.y. MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za alizeti kwa wakulima ili kuzalisha mafuta ya kula?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbuge wa Kawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kuwa, nchi yetu inazalisha alizeti itakayo changia kwa kiasi kikubwa katika kuzalisha mafuta ya kula na kuokoa fedha za kigeni zinazotumika kuagiza mafuta ya kula, Serikali imepanga kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti kwa kuongeza uzalishaji wa mbegu bora kutoka tani 1,500 zilizokuwepo awali hadi tani 5,000 kwa lengo la kuongeza eneo kubwa zaidi la uzalishaji wa alizeti ili kuweza kufikia malengo; Kuendelea kutekeleza mkakati wa uandaaji wa mashamba makubwa zikiwemo block farms ambayo kwa asilimia kubwa yatatumiwa na wakulima kwa kilimo cha alizeti; na Wakala wa Mbegu (ASA) tayari ameanza usambazaji wa mbegu bora ya alizeti aina ya record ambayo imethibitishwa ubora na inauzwa kwa bei ya ruzuku ili kuhakikisha kwamba inamletea tija mkulima.