Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 82 2022-11-07

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha upatikanaji wa soko la machungwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma, Mbunge wa Jimbo la Muheza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha upatikanaji wa masoko ya uhakika ya machungwa ambayo huzalishwa kwa wingi katika Mkoa wa Tanga hususan Wilaya ya Muheza, Wizara kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeendelea kutafuta masoko katika nchi mbalimbali, ambapo mwaka 2021/2022 liliweza kupatikana soko la machungwa katika nchi za falme za Kiarabu. Vile vile, Serikali inaendelea kutoa elimu ya ufungashaji na usindikaji wa matunda ya aina zote kwa wazalishaji ili kuyaongezea thamani na kuweza kunufaika na fursa hiyo ndani ya nchi ambayo itaongeza soko kwa matunda yakiwemo machungwa. Nakushukuru sana.