Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 80 2022-11-07

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Askari Wanyamapori katika Wilaya ya Itilima na maeneo yanayozunguka Pori la Akiba Maswa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Jimbo la Itilima, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara imekamilisha ujenzi wa Kituo cha Askari Wanyamapori katika Wilaya ya Itilima mwezi Oktoba, 2022. Kituo hicho kipo katika Kijiji cha Longalombogo ambapo kitakuwa na Askari wa Jeshi la Uhifadhi na Askari Wanyamapori wa Vijiji (VGS) na kitahudumia zaidi ya vijiji tisa vikiwemo Longalombogo, Nding’ho, Lung’wa, Nyantugutu, Mbogo, Shishani, Pijulu, Ng’walali na Mwamakili.