Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Madini 77 2022-11-07

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wanawake wanakuwa wachimbaji wa madini nchini?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia STAMICO ina jukumu la kuwasadia wachimbaji wadogo wa madini wa makundi mbalimbali nchini wakiwemo wanawake. Aidha, STAMICO imeandaa na kutekeleza mikakati mbalimbali kuhakikisha wanawake pia wanakuwa wachimbaji madini nchini.

Mheshimiwa Spika, mikakati hiyo inahusisha, pamoja na mambo mengine, kutoa mafunzo mbalimbali ya nadharia na vitendo kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wanawake kupitia vituo vya mfano tulivyonavyo katika maeneo ya Katente (Bukombe), Lwamgasa (Geita) na Itumbi (Mbeya); kuwasaidia wachimbaji wadogo kupata taarifa sahihi za mashapo kwa kushirikiana na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) ambapo kwa sasa STAMICO imeagiza mitambo mitano ya uchorongaji maalumu kwa ajili ya wachimbaji wadogo nchini ili kuwasaidia kufanya utafiti.

Mheshimiwa Spika, mkakati mwingine ni kuwaunganisha wachimbaji na taasisi za Kifedha zikiwemo Benki za CRDB, NMB na KCB kwa lengo la taasisi hizo kuweza kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo nchini wakiwemo wanawake. Ahsante sana.