Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 75 2022-11-07

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo kidogo cha Polisi cha Chaani Lungalunga.?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Chaani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo kidogo cha Polisi cha Chaani, Lungalunga kilichopo Wilaya ya Kaskazini A ni kituo kilichojengwa kwa kushirikisha jitihada na nguvu za wananchi. Jengo la kituo hiki ni chakavu na haliwezi kufanyiwa ukarabati kwa sababu kuta zake zimeweka nyufa nyingi na kingo za jengo zimebomoka.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi Kamisheni ya Zanzibar imeshaandaa mchoro na makadirio kwa ajili ya kujenga Kituo kipya cha Daraja C katika eneo hilo. Kiasi cha fedha, shilingi 82,530,960 kinahitajika kwa ajili ya ujenzi huo, na zitaingizwa katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 kulingana na upatikanaji wa fedha. Nashukuru.