Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 70 2022-11-07

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza: -

Je, ni kwa kiwango gani Mbunge anashirikishwa katika miradi inayoibuliwa na wananchi katika Jimbo lake kupitia TASAF?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa, Mbunge wa Mtambwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uibuaji wa miradi ya jamii inayochangiwa na TASAF hufanyika kwenye mikutano ya jamii ambayo huendeshwa na wataalam chini ya usimamizi wa viongozi wa maeneo hayo. Mbunge au Mwakilishi wa eneo husika kama anakuwepo wakati zoezi la kuibua miradi likifanyika hazuiwi kushiriki kwa kuwa hakuna mwongozo unaomtaka Mbunge asiwepo wakati wa zoezi la kuibua miradi.

Mheshimiwa Spika, wananchi huibua miradi ambayo inatatua kero walizonazo katika jamii kutokana na kukosekana kwa huduma stahiki. Ikiwa wananchi wote kwenye mkutano wameridhia mradi fulani kutekelezwa, basi moja kwa moja huo unakuwa ni chaguo lao. Lakini kama kuna miradi miwili au mitatu iliyopendekezwa, jamii hupiga kura na mradi utakaopata kura nyingi ndio unapewa kipaumbele cha kuanza kutekelezwa. Jamii ikishaamua mradi wa kutekeleza, timu ya Wataalam hufanya bajeti ya mradi huo na kurudi tena kwa wananchi kukubaliana kuhusu mchango wa jamii kabla bajeti hiyo haijawasilishwa TASAF kwa hatua nyingine.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.