Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 67 2022-11-07

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga uzio na uwanja wa michezo katika Shule Maalum ya Watoto wa kike Asharose migiro iliyopo Wilayani Mwanga?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athuman Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa michezo na utamaduni katika ukuaji na maendeleo ya wanafunzi na kutazama michezo na sanaa kwa mlengo wa ajira na stadi muhimu zinazochangia ukuaji wa kiuchumi na kijamii, Serikali imedhamiria kuboresha miundombinu ya michezo katika Shule teule 56 nchini ikiwa ni wastani wa shule mbili kwa kila mkoa.

Mhesahimiwa spika, Shule ya Sekondari Asharose Migiro haipo kwenye mpango wa shule za sekondari zilizochaguliwa kuwa za michezo hivyo, inashauriwa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kutenga fedha kwenye Bajeti yake ya mapato ya ndani ili kuanza ujenzi wa uzio katika viwanja hivyo.