Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 64 2022-11-04

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL T. AWACK aliuliza: -

Je, ni lini itatolewa bei elekezi ya maji katika Karatu ili kuondoa tofauti kati ya KARUWASA wanaouza unit 1 Sh.1,700 na KAVIWASU unit 1 Sh.3,000?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Tlemai Awack, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha hakuna changamoto katika ulipaji wa bili za maji kwa wananchi. Hivyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023, imeviunganisha vyombo vya usimamizi wa huduma ya maji KARUWASA na KAVIWASU na kuunda chombo kimoja cha KARUWASA ambacho kitakuwa imara ili kiweze kutoa huduma ya maji kwa ufanisi katika eneo lote la Mji wa Karatu.

Mheshimiwa Spika, bei elekezi ya kuanzia kwa uniti moja ya maji imeshatolewa na inatumika. Aidha, marekebisho yataendelea kufanyika kwa kuzingatia miongozo kutoka EWURA.