Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 52 2022-11-04

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kumaliza mgogoro kati ya Wananchi na Wawekezaji wenye leseni ya uchimbaji madini Kata ya Guta – Bunda?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mgogoro uliopo unahusisha wamiliki wa mashamba waliojichukulia haki madini (Mineral Rights) bila kufuata sheria kwenye eneo ambalo leseni zilikwishatolewa kwa mwekezaji aitwaye JB & Partners ambaye alipewa leseni ndogo za uchimbaji (PMLs) nane (8). Leseni hizi zimo ndani ya mashamba 21 ya wakazi wa maeneo ya Mtaa wa Stooni, Kata ya Guta Wilaya ya Bunda. Mpango uliopo ili kumaliza mgogoro huo ni kuendelea na majadiliano ili kufikia maridhiano kati ya wamiliki wa mashamba hayo na mwekezaji aliyepewa leseni. Hadi sasa kupitia majadiliano wamiliki wa leseni wamekwishaingia maridhiano na kusaini makubaliano ya uchimbaji kwa ubia na wamiliki wa mashamba 13 kati ya 21 wanaotambulika katika eneo hilo la uchimbaji.

Mheshimiwa Spika, kwa mashamba 13 mgogoro wake ulifika tamati na machimbo kufunguliwa na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mara mnamo tarehe 6 Oktoba, 2022 na shughuli za uchimbaji zinaendelea. Wamiliki wa mashamba nane waliobaki waliogoma kufanya majadiliano na walifungua kesi ya ardhi (Land Case No. 12 of 2021) katika Mahakama ya Musoma ambayo inaendelea kusikilizwa. Hata hivyo, wamiliki wa mashamba hayo nane wamepatiwa nafasi nyingine ya majadiliano na katika maeneo yao uchimbaji umesimamishwa hadi pale watakaporidhiana. Endapo watashindwa kuridhiana ndani ya muda uliowekwa kwa mara nyingine basi taratibu nyingine za kisheria zitafuatwa kwa mujibu wa Kifungu cha 97 cha Sheria ya Madini, Sura 123. Ahsante sana.