Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 51 2022-11-04

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, kuna Mkakati gani wa kukabiliana na mafuriko katika Mto Mbezi yanayosababisha uharibifu wa miundombinu ya shule na makazi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto mbalimbali zinazotokana na mafuriko katika mito yetu nchini ukiwemo Mto Mbezi. Kwa kutambua changamoto hiyo, Serikali imeandaa Mwongozo wa usafishaji mchanga, tope na taka ngumu kwenye mito na mabonde katika Mkoa wa Dar es Salaam wa Mwaka 2021. Mwongozo huu unalengo la kuzitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kusafisha tope na mchanga kwenye mito na mabonde ili kuruhusu uwepo wa mtiririko mzuri wa maji kuelekea baharini ili kuepuka athari za mafuriko.

Mheshimiwa Spika, Serikali inapenda kumhakikishia Mbunge kuwa, itaendelea kuimarisha utekelezaji wa Mwongozo ili kutatua changamoto ya mafuriko katika mito na mabonde yaliyopo katika Mkoa wa Dar es Salaam ili kukabiliana na madhara ya mafuriko na kuhakikisha miundombinu ya shule na makazi ya watu yanaendelea kuwa salama. Nakushukuru.