Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 48 2022-11-03

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, ni lini RUWASA Nyasa itapatiwa gari ili kurahisisha utendaji kazi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI k.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eng. Stella Martin Manyanya Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuijengea uwezo RUWASA Mkoa wa Ruvuma ili iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya magari 86 yatanunuliwa na kupelekwa kwenye Wilaya mbalimbali nchini ikiwemo Wilaya ya Nyasa. Ahsante.