Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 44 2022-11-03

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuitanua sehemu ya kusafirishia abiria wanaokwenda Zanzibar katika Bandari ya Dar es Salaam?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Haji Kassim, Mbunge wa Mwanakwerekwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia TPA imetenga kiasi cha Sh.1,500,000,000 kwa ajili ya maboresho ya sehemu ya abiria katika Bandari ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, hatua iliyofikiwa sasa ni manunuzi ya Mkandarasi kwa ajili ya maboresho ya eneo la kusafirisha abiria kwenda Zanzibar. Maboresho yatahusisha ukarabati wa miundombinu ya gati la kuhudumia abiria ikiwa ni pamoja na ujenzi wa jengo jipya la abiria ili kuongeza uwezo wa kuhudumia abiria, kuweka mkanda wa mizigo (conveyor belt), ukarabati wa kingo za gati, maboresho ya sehemu ya abiria mashuhuri (VIP), sakafu na vyoo. Aidha, Mkandarasi anatarajiwa kupatikana na kuanza kazi mwezi wa Desemba, 2022.