Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 39 2022-11-02

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, kuna mpango gani kuweka Mazingira bora ya uwekezaji kilimo cha Michikichi pamoja na kiwanda cha kuchakata mafuta – Kigoma?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Felix, Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuongeza uzalishaji wa mbegu za michikichi, Serikali imeanzisha Kituo Maalum cha Utafiti wa Zao la Michikichi cha TARI Kihinga, mkoani Kigoma ili kuendeleza zao hili kwa ufanisi. Vile vile, Serikali kupitia Wizara yangu, imepanga kujenga viwanda viwili vidogo vya kuzalisha mafuta ya mawese katika Kijiji cha Nyamuhoza kilichopo Wilaya ya Kigoma (DC) na Kijiji cha Sunuka kilichopo Wilaya ya Uvinza.

Mheshimiwa Spika, juhudi zote hizo zimelenga kuweka mazingira bora ya uwekezaji kwenye zao la michikichi mkoani Kigoma.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.