Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 38 2022-11-02

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa maji wa Mkwiti utakamilika ili kupunguza tatizo la maji katika Kata ya Mangombya, Mkwiti na Litehu?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmed Katani Mbunge wa Tandahimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Mkwiti utakaohudumia Kata za Mangombya, Mkwiti na Litehu zenye jumla ya vijiji 16. Mradi huu unatekelezwa kwa awamu nne ambapo awamu ya kwanza na ya pili zimekamilika na ilihusisha ujenzi wa bomba kuu lenye urefu wa kilometa 13 na ufungaji wa pampu kwenye chanzo. Utekelezaji wa awamu ya tatu na ya nne unaendelea na umefikia asilimia 50 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022. Kazi zinazofanyika ni pamoja na ujenzi wa matanki sita yenye jumla ya ujazo wa lita 300,000, ulazaji wa bomba lenye urefu wa kilomita 89 na ujenzi wa vioski 48 vya kuchotea maji. Ahsante.