Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 37 2022-11-02

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Bandari Kavu katika Mkoa wa Kigoma?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Bandari Kavu umepewa kipaumbele katika Mpango Kabambe wa Mamlaka ya Bandari Tanzania ulioanza 2009 na utaisha 2028. Mpango huo umeziainisha Bandari Kavu za King’ori iliyoko mkoani Arusha, Ihumwa (Dodoma), Inyala (Mbeya), Shinyanga (Isaka), Fela (Mwanza), Katosho (Kigoma), Kwala (Pwani) na Songea kuwa bandari za kipaumbele kutokana na matarajio ya kuongezeka kwa shehena katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia TPA imetenga fedha kwa ajili kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa bandari hizo ikiwemo ya Katosho ilioko mkoani Kigoma. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu inatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2023. Kukamilika kwa kazi hiyo kutapelekea manunuzi ya Mkandarasi wa ujenzi wa bandari hiyo ambayo ni muhimu kwa kuhudumia shehena za nchi jirani za ukanda wa Ziwa Tanganyika. Ahsante.