Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 35 2022-11-02

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, ni lini Benki Kuu itaweka utaratibu mzuri kwa Serikali na taasisi zake kuweka fedha katika Benki za biashara ili kuwa na mzunguko mzuri wa fedha?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa sasa wa Serikali na taasisi zake kutunza fedha za Benki Kuu ni mzuri na wa uwazi zaidi kwa kuwa unachochea ukuaji wa huduma jumuishi za kifedha. Aidha, mfumo wa sasa unaiwezesha Serikali kusimamia kwa ufanisi utulivu wa uchumi jumla, hususan sarafu yetu na mfumuko wa bei nchini ambao ni msingi wa ukuaji endelevu wa uchumi jumuishi. Vilevile, utaratibu wa sasa unatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania, Sura ya 197. Ahsante sana.