Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 32 2022-11-02

Name

Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kunusuru maisha ya vijana wa kike kwa kudhibiti wimbi la mauaji Visiwani Zanzibar?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saada Mansour Hussein, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kufuatilia kwa karibu matukio ya mauaji yanayotokea maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo Zanzibar. Matukio haya tumebaini yanasababishwa na migogoro ya ardhi, wivu wa kimapenzi na migogoro ya ndoa, imani za kishirikiana, wananchi kujichukulia sheria mikononi, ulevi, na matukio ya uhalifu.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Oktoba 2022 jumla ya matukio manne (4) ya mauaji ya wanawake yametokea Zanzibar. Matukio haya yamehusishwa na wivu wa mapenzi na migogoro katika ndoa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itaendelea kutoa elimu kwa jamii kufuata sheria za nchi na njia sahihi za kutatua migogoro ya aina hiyo. Tunawashauri wahusika kuzishirikisha familia zao, viongozi wa dini, viongozi wa jamii, viongozi wa siasa, wazee wa mila, watu maarufu na wenye ushawishi katika jamii pamoja na Ofisi za Serikali za Mitaa ili kupunguza athari za migogoro hiyo. Aidha, kwa migogoro inayoshindikana ifikishwe katika vyombo vya dola hususan Polisi na Mahakama ili kupata suluhisho la kisheria.