Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 29 2022-11-02

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: -

Je, Serikali ina taarifa juu ya upatikanaji wa madini Nanyumbu na Je, wananchi wananufaikaje?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kwa Niaba ya Waziri wa Madini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Taasisi yake ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), ilifanya utafiti wa awali katika Wilaya ya Nanyumbu iliyopo kwenye Quarter Degree Sheet (QDS) 316 na kubaini uwepo wa madini mbalimbali. Utafiti huo ulionesha kuwepo kwa madini ya dhahabu katika vijiji vya Lukwika, Chungu, Chipuputa na Masuguru. Katika kijiji cha Masuguru utafiti huo ulibaini pia uwepo wa madini ya sapphire, Acquamarine na rhodolite. Aidha, Wilaya ya Nanyumbu imebainika kuwa na madini mengine yakiwemo madini ujenzi.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini katika Wilaya ya Nanyumbu imetoa leseni za uchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu 73, madini ya chuma nane, madini ujenzi mbili, madini ya vito 10 na leseni mbili za utafutaji wa madini ambapo moja ni kwa ajili ya utafutaji madini ya nikeli na nyingine ni kwa ajili ya madini ya dhahabu. Aidha, katika maeneo hayo shughuli za utafiti na uzalishaji zinaendelea. Kufuatia shughuli hizo wananchi wamekuwa wakijipatia kipato, ajira na mzunguko wa biashara kuwepo katika vijiji hivyo.

Mheshimwa Spika, ahsante sana.