Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 28 2022-11-02

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha matokeo ya tafiti za kilimo yanawafikia wakulima?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Mwita Kembaki, Mbunge wa Tarime, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha matokeo ya tafiti za kilimo yanawafikia wakulima, Taasisi za Utafiti na Idara ya Ugani hutumia njia mbalimbali kufikisha taarifa za utafiti na matumizi ya teknolojia ambazo ni pamoja na kufungua mashamba darasa na mashamba mfano katika maeneo ya kilimo, kutengeneza na kusambaza majarida ya tafiti za kilimo, uwezeshaji wa shughuli za ugani, kuwepo kwa siku ya mkulima, warsha kwa wadau, ushirikishwaji wa wakulima kwenye tafiti na kukusanya takwimu za kiutafiti.

Mheshimiwa Spika, vilevile, safari za mafunzo, vituo mahiri na atamizi vya uhaulishi teknolojia katika viwanja vya Nanenane, maonesho ya kilimo na biashara, vyombo vya habari, mitandao ya kijamii. Vilevile simu za kiganjani, maandiko ya kisayansi na machapisho.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 Taasisi za Utafiti zimeshiriki katika maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa Jijini Mbeya katika Kiwanja cha John Mwakangale na Viwanja vingine vya Kikanda.