Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 18 2022-11-01

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa kufua umeme wa upepo na jua wa MW 100 utaanza rasmi katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhan, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwekezaji aitwaye Upepo Energy alifanikiwa kushinda zabuni ya kuendeleza miradi miwili ambapo Megawatt 100 za umeme zitazalishwa kwa nguvu ya upepo na Megawatt 45.08 zitazalishwa kwa nguvu ya jua.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa majadiliano baina ya TANESCO na Mwekezaji kuhusu bei ya kuuziana umeme (PPA) yamekamilika. Majadiliano kuhusu mkataba wa utekelezaji (Implementation Agreement-IA) yanaendelea. Ipo changamoto ya mwekezaji kuhitaji “Government Guarantee” kinyume na Sera ya Serikali na masharti ya zabuni kama ilivyotangazwa. Iwapo mwekezaji atakubali kutekeleza mradi huu bila masharti mapya aliyoweka, mradi huu utaanza kutekelezwa mwezi Januari, 2023.