Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 14 2022-11-01

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: -

Je, ni lini Ofisi ya TRA itajengwa katika Halmashauri ya Kibondo ili kuzuia biashara holela katika masoko ya ujirani mwema kati ya Tanzania na Burundi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, TRA ilifanya utafiti katika maeneo yote nchini yenye uhitaji wa ofisi za kudumu za usimamizi wa kodi ikiwemo Halmashauri ya Kibondo na kubaini kuwa gharama za usimamizi wa kodi katika Wilaya ya Kibondo zitakuwa kubwa ikilinganishwa na kiwango cha kodi kinachotarajiwa kukusanywa. Kwa muktadha huo, TRA itaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa ukuaji wa shughuli za kiuchumi na ukusanyaji wa kodi katika wilaya hiyo ili mara tu itakapokidhi vigezo, TRA itafungua ofisi za kudumu. Aidha, TRA itaendelea kuimarisha mfumo wa sasa wa kuhudumia walipakodi wa Wilaya ya Kibondo ili kuwawezesha kulipa kodi bila usumbufu wowote. Ahsante.