Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 12 2022-11-01

Name

Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Primary Question

MHE. YAHYA ABDULWAKIL AHMED aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ununuzi wa meli nane za uvuvi itatekelezwa?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI aljibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Abdulwakil Ahmed, Mbunge wa Kwahani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali, naomba nifanye maboresho madogo sana katika aya inayosema katika mwaka wa fedha 2023/2024, badala yake isomeke katika mwaka wa fedha 2022/2023 Mheshimiwa Spika, baada ya maboresho hayo, naomba niendelee sasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea na hatua mbalimbali za ununuzi wa meli nane (8) za Uvuvi katika Bahari Kuu kama alivyoagiza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza agizo hilo Serikali itanunua meli nane kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) chini ya Mfuko wa Kimataifa wa Kuendeleza Kilimo-IFAD kwa awamu mbili ambapo katika mwaka wa fedha 2023/2024, meli nne na vifaa vyake zitanunuliwa. Meli hizo zitagawanywa Tanzania Bara meli na Zanzibar meli.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Mkataba baina ya Serikali na IFAD ununuzi wa meli hizo unatakiwa kukamilika baada ya kufanyika kwa tathmini ya athari za kimazingira na kijamii pamoja upembuzi wa kina wa uendeshaji wa meli za uvuvi. Hata hivyo, taratibu za kufanya Upembuzi huu yakinifu zinaendelea. Ahsante.