Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 8 2022-11-01

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kumaliza tatizo la maji safi na salama Wilaya za Newala, Tandahimba na Nanyumbu Mkoani Mtwara?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji 26 ambapo miradi 14 imekamilika na miradi 12 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Aidha, Serikali imeanza ujenzi wa mradi wa maji wa miji 28, ambapo Mkoa wa Mtwara miradi inayotekelezwa ni mradi wa maji Makonde na Nanyumbu. Utekelezaji huu unatarajiwa kukamilika mwezi Februari, 2024 na utanufaisha wananchi zaidi ya 500,000 wa Wilaya za Newala, Tandahimba na Nanyumbu.