Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 36 2022-09-14

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalinda watumiaji wa cyanide kama mbadala wa zebaki?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatumia njia mbalimbali kuwalinda watumiaji wa cyanide kuzuia athari za kiafya zisitokee wakati wa kutumia kemikali hizi ikiwa ni pamoja na: -

(a) Kuelimisha wachimbaji juu ya madhara yanayotokana na matumizi ya cyanide na namna ya kujikinga na madhara yake. Pia kuwaelimisha kufika vituo vya kutolea huduma za afya mapema kupata matibabu wanapopata madhara.

(b) Kufanya upimaji wa afya za wafanyakazi maeneo ya migodini.

(c) Kutumia njia nyingine katika uzalishaji wa dhahabu katika migodi iliyopo hapa nchini kama direct smelting na njia nyingine mbadala.