Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 34 2022-09-14

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu Kata ya Jangwani na Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Selemani Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Jangwani iliyopo katika Manispaa ya Mtwara Mikindani inapata huduma za mawasiliano kutoka kwa Kampuni za Tigo, Airtel na Vodacom. Vile vile maeneo ya Kata ya Mtawanya yanapata huduma hafifu za mawasiliano kutoka kwa watoa huduma wa Airtel, Vodacom na Tigo kupitia minara iliyojengwa katika Kata ya Likombe juu ya Mlima wa Lilungu.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote itavifanyia tathmini na uhakiki wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano maeneo yote yaliyopo katika Kata za Jangwani na Mtawanya na kuchukua hatua stahiki mara moja ili kuimarisha na kuboresha huduma endapo utatuzi hautahitaji ujenzi wa minara mipya.

Mheshimiwa Spika, endapo tathmini hiyo itabaini utatuzi wa changamoto zilizopo unahitaji ujenzi wa minara mipya, maeneo husika katika kata hizi yataainishwa na kuingizwa katika zabuni za kufikisha huduma ya mawasiliano zitakazotangazwa katika mwaka wa fedha 2023/2024. Ahsante.