Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 28 2022-09-14

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuweka miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu katika vyombo vya usafiri ikiwemo mabasi ya mwendokasi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantatu Mbarak Khamis Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikisimamia upatikanaji wa huduma bora na salama kwa watumiaji wa usafiri kwa makundi yote ya jamii wakiwemo wenye ulemavu. Serikali imekuwa ikizingatia mahitaji ya makundi maalum hasa wenye ulemavu katika ujenzi wa miundombinu ya usafiri ikiwemo miundombinu ya mabasi ya mwendokasi.

Mheshimiwa Spika, miundombinu ya mabasi ya mwendokasi inayotumika sasa na inayoendelea kujengwa imezingatia watu wenye mahitaji maalumu. Aidha, mabasi yote ya mwendo kasi yamezingatia watu wenye mahitaji maalumu hususan wenye ulemavu, wazee na wajawazito. Ahsante.