Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 23 2022-09-14

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY K.n.y. MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti wa kujua sababu za kusambaa kwa maji ya Ziwa Bassuto na kuhama kwa samaki kwenye Ziwa Eyasi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujiibu swali la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Hanang kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali imeona hakuna haja ya kufanya utafiti wakujua sababu ya kusambaa kwa maji na kuhama kwa samaki ziwa Bassuto. Sababu kuu ni kujaa maji wakati wa mvua nyingi, ziwa hilo ni dogo halina uwezo wa kuhifadhi maji mengi yanayosababishwa na mvua nyingi. Aidha, maji hayo hutawanyika na kuingia Ziwa Eyasi na kwa kuwa Ziwa Bassuto lina viumbe mbalimbali ikiwemo samaki, maji hayo yanapoingia kwenye Ziwa Eyasi huingiza na viumbe mbalimbali wanaoishi kwenye Ziwa Bassuto ikiwemo samaki. Hali hii inasababisha wananchi wanaotegemea samaki wa Ziwa Bassuto inawabidi kupata samaki hao kwenye Ziwa Eyasi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatoa wito kwa viongozi wa Wilaya ya Hanang kuendelea kuhamasisha wananchi kuhifadhi vyanzo vya maji ikiwemo Maziwa ya Bassuto na Ziwa Eyasi.