Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 45 2022-09-15

Name

Maulid Saleh Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MAULID SALEH ALI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzuia Hati za kusafiria kwa Wakandarasi wanaoingia nchini kutekeleza miradi mbalimbali?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, Mbunge wa Welezo, kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, Serikali haina mkakati wa kuzuia hati za kusafiria kwa Wakandarasi wanaoingia nchini kutekeleza miradi mbalimbali isipokuwa inafanya hivyo kwa mujibu wa sheria pale inapohitajika. Serikali kupitia Sheria ya Uhamiaji Sura Na. 54 rejeo la mwaka 2016, imeipa mamlaka Idara ya Uhamiaji kuweza kushikilia au kuzuia kitu chochote ikiwa ni pamoja na nyaraka yoyote ambayo inaweza kuonyesha au kuthibitisha uvunjifu wa sheria.