Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 51 2022-09-16

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE ANTON A. MWANTONA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati majengo ya Zahanati ya Ukoma kuwa Kituo cha Afya cha Kata ya Kisondela Wilayani Rungwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Majengo ya Zahanati ya Makete, Ukoma yaliyokuwa yakitumika kwa wagonjwa wa ukoma ni chakavu. Aidha, kwa kuwa eneo la Kata hii halikidhi vigezo vya kuwa na Kituo cha Afya cha Kimkakati kwa kuzingatia idadi ya watu wasiofikia angalau 10,000, Serikali itaendelea kuitumia zahanati inayotumia moja ya majengo haya kutoa huduma kwa wananchi wa eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kata hiyo itakapokidhi vigezo vya kuwa na Kituo cha Afya cha kimkakati, Serikali itafanya maamuzi stahiki. Ahsante.