Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 21 Energy and Minerals Wizara ya Madini 176 2016-05-17

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY T. MAYENGA (K.n.y. MHE. SALOME W. MAKAMBA) aliuliza:-
Tatizo la kukatika umeme mara kwa mara katika Jimbo la Kahama Mjini linaathiri sana uzalishaji viwandani hasa ukizingatia Serikali imepiga marufuku kwa baadhi ya viwanda kama vile vya kukoboa mpunga na kusaga mahindi kutofanya kazi usiku:-
Je, Serikali ipo tayari kuruhusu viwanda Wilayani Kahama kufanya kazi masaa 24 ili kufidia uzalishaji unaokuwa haufanyiki kipindi umeme unapokuwa umekatika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salome Wycliffe Makamba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa hakuna zuio lolote la Halmashauri ya Mji wa Kahama kwamba mashine za kukoboa mpunga na mahindi zisifanye kazi wakati wa usiku au saa 24. Changamoto iliyopo ni kwamba viwanda hivyo vinatumia umeme wa jenereta ambao hautoshelezi kuendesha mashine wakati wote, hivyo kumekuwa na tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara. Halmashauri imewasiliana na Meneja wa TANESCO Kahama na tayari tatizo hilo limeanza kushughulikiwa ili kupata umeme wa uhakika kutoka gridi ya Taifa ambapo tayari kituo cha usambazaji kimeanza kujengwa Kahama.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri inahamasisha wawekezaji wa viwanda vidogo, vikiwemo vya kukoboa mpunga, mahindi na mazao mengine ili kupanua wigo wa mapato kupitia ushuru wa huduma (service levy) na ajira kwa vijana, hivyo hakuna sababu yoyote kwa Serikali kuzuia wawekezaji katika viwanda vidogo na vikubwa. Azma ya Serikali ni kupanua uwekezaji wa viwanda kadri iwezekanavyo kwa kuzingatia fursa zilizopo. Tunachofanya ni kuboresha mazingira yatakayosaidia uwekezaji huo ufanyike kwa faida, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha umeme wa uhakika unakuwepo.