Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 82 2022-09-19

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuza: -

Je, Serikali inaweza kutoa idadi na aina ya mikopo ya Zanzibar baada ya makubaliano na kuiwezesha Zanzibar kukopa yenyewe?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Mwera, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa kifungu cha 15 cha Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada, Sura 134, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepewa mamlaka ya kupokea misaada yenyewe kutoka kwa Washirika wa Maendeleo. Kwa mujibu wa kifungu cha 3 na 13, mamlaka ya kukopa na kutoa dhamana yamewekwa chini ya Waziri wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na anaweza kuyakasimu kwa Waziri wa Fedha wa SMZ baada ya kushauriwa na Kamati ya Kitaifa ya Madeni yenye Wajumbe toka pande zote mbili za Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, yaani 2019/2020 - 2021/2022, thamani ya mikataba ya mikopo kutoka vyanzo vya nje iliyosainiwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya SMZ ikiwemo barabara, afya, elimu na mapambano dhidi ya janga la UVIKO-19 ni takribani shilingi trilioni 1.1. Ahsante.