Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 80 2022-09-19

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kurekebisha ramani ya nchi yetu baada ya baadhi ya maeneo kujazwa mchanga kuongeza ukubwa wa ardhi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi naomba kujibu swali namba 80 la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kujibu swali la msingi la Mheshimiwa Mbunge, napenda kutoa maelezo mafupi kuwa, ukubwa wa eneo na mipaka ya nchi unajulikana na ipo bayana. Hivyo kujazwa mchanga kwenye baadhi ya maeneo hakuongezi wala kupunguza ukubwa wa eneo la nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ramani ya nchi inaonesha sura ya nchi huandaliwa ili kuonyesha hali halisi iliyopo ardhini ikijumuisha taarifa za kijiografia za asili ambazo ni pamoja na mito, maziwa, milima na bahari; na zile zisizo za asili ambazo zinazojumuisha barabara, reli, mabwawa na miji. Moja ya sababu ya kuhuisha ramani ni kuonesha uhalisia wa sura ya nchi na kuhakikisha kuwa mabadiliko yanayotokea katika ardhi yanaoneshwa kwenye ramani mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ina mpango wa kuandaa ramani mpya nchi nzima zinazoonesha sura ya nchi Tanzania Bara. Ramani hizo zitaandaliwa kupita mipaka kupitia Mradi wa Kuimarisha Miundombinu ya Upimaji na Ramani (Project for Improvement of National Land Data Infrastructure) utakaotekelezwa kwa mkopo utakaotolewa na Serikali ya Korea kwa muda wa miaka minne (2022/23 -2025/2026).