Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 175 2016-05-17

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:-
Mkoa wa Simiyu ulianzishwa kisheria na Makao Makuu yake kuwa kwenye Mji Mdogo wa Bariadi badala ya Mji wa Maswa:-
(a) Je, ni vigezo gani vilitumika kuamua Makao Makuu ya Mkoa na shughuli zake yawe Bariadi badala ya Maswa ambako kuna majengo ya kutosha ya Serikali; badala yake Serikali inaingia kwenye matumizi makubwa ya kupanga ofisi toka nyumba za watu binafsi huko Bariadi?
(b) Je, Serikali inaweza kufikiria kubadilisha maamuzi haya kwa manufaa ya Taifa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, maamuzi ya Makao Makuu ya Mkoa wa Simiyu kuwa Bariadi Mjini siyo Maswa yalipitishwa na wananchi wenyewe kupitia vikao vya kisheria ambavyo ni Mkutano Mkuu wa Vijiji, Kamati za Maendeleo ya Kata, Mabaraza ya Madiwani, Kamati za ushauri za Wilaya (DCC) na Mkoa (RCC). Uamuzi wa mwisho ulifanyika katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa tarehe 10 Mei, 2010 ambapo Wajumbe wote waliridhia pendekezo la Bariadi Mjini kuwa Makao Makuu ya Mkoa wa Simiyu. Hivyo, kigezo kikubwa kilichotumika kuamua Makao Makuu kilikuwa ni maamuzi ya pamoja kupitia vikao halali vilivyoshirikisha wadau kutoka Wilaya zote, wakiwemo kutoka sekta binafsi.
(b) Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika sehemu ya (a) ya jibu hili, maamuzi hayo yalifanywa na vikao halali vya kisheria, ikiwahusisha Wajumbe wa vikao hivyo, hivyo kitendo cha Serikali kubadilisha maamuzi hayo itakuwa ni kuwanyang‟anya madaraka wananchi yaliyowekwa kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 145.