Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 74 2022-09-19

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: -

Je, kuna Wavumbuzi wangapi na wa teknolojia gani kwani Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Taifa una lengo la kuchochea uvumbuzi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mchango wa uvumbuzi na ubunifu kama nyenzo muhimu katika kuchochea ushindani na uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya watu kama ilivyoainishwa kwenye Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuibua, kutambua na kuendeleza uvumbuzi, ubunifu na maarifa asili ya Tanzania kupitia mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) na programu ya kutambua teknolojia zinazozalishwa ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa Serikali imetambua wavumbuzi na wabunifu wapatao 2,735 katika sekta za Afya, Viwanda, Elimu, Kilimo, TEHAMA, Usafirishaji, Nishati, Madini, Mazingira, na Uvuvi. Aidha, Teknolojia 479 zimeweza kuibuliwa, kutambuliwa na kuhakikiwa. Wabunifu 376 wanaendelezwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Kati ya bunifu zilizoendelezwa, 35 zimefikia hatua za ubiasharishaji. Ninakushukuru sana. (Makofi)