Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 73 2022-09-19

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza wigo wa biashara baina ya Zanzibar na Tanzania Bara ili kuongeza mapato?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Said Issa, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ina Mipango na Mikakati mbalimbali ili kuendelea kupanua wigo wa Biashara baina ya Tanzania Bara na Zanzibar ikiwemo: -

(i) Kuendelea kutoa elimu na kuongeza hamasa zaidi kwa makampuni ya Tanzania Bara na Zanzibar kushiriki katika Maonesho mbalimbali yanayofanyika ndani ya Tanzania Bara na Zanzibar;

(ii) Kufanya tathmini na kubaini vizuizi visivyo vya kikodi;

(iii) Kuzishirikisha Mamlaka mbalimbali ikiwemo Mamlaka za Mapato za Tanzania Bara (TRA) na Zanzibar (ZRA) kwenye majadiliano ya pamoja ili kupanua wigo wa Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Upanuzi wa ushirikiano wa kibiashara unazingatia na kuheshimu sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Ninakushukuru.