Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2022-09-19

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha za ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Ukata na Litumbandyosi, Halmashauri ya Wilaya Mbinga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka Shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi Kituo cha Afya cha Kimkakati katika Kata ya Mkumbi iliyopo Tarafa ya Mkumbi. Kituo hiki cha kimkakati kitahudumia Kata sita (6) za tarafa hiyo ikiwemo Kata ya Ukata. Ujenzi wa Kituo hicho cha Afya upo katika hatua za umaliziaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga katika mwaka 2022/2023, imetenga Shilingi milioni 500 fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Litumbandyosi.