Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 89 2022-09-20

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, ni nini tamko la Serikali kuhusu uchimbaji unaoendelea katika Mto Nyandurumo ambao ni chanzo cha maji kwa wakazi wa Tarime?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, chanzo cha maji cha Nyandurumo ni chanzo ambacho kinatoa huduma ya maji kwa Mji wa Tarime ambapo kina uwezo wa kuzalisha maji lita 6,000,000 kwa siku kwa kipindi cha masika na lita 1,500,000 kwa kipindi cha kiangazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na uharibifu unaojitokeza kwenye chanzo hicho, Serikali kupitia Watalaam wa Mazingira wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Bonde la Ziwa Victoria na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara wamewaondoa wachimbaji waliokuwa wanafanya shughuli za kusafisha madini karibu na chanzo hicho cha maji na kupanda miti 205 ambayo ni rafiki kwa mazingira ikiwa na lengo la kulinda na kuhifadhi chanzo hicho. Umbali wa kutoka maeneo ya uchimbaji hadi kwenye chanzo cha maji ni takribani kilometa tatu.