Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 6 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 88 2022-09-20

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Mwekezaji wa Kiwanda cha Saruji katika Wilaya ya Uvinza?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Vieanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ili kuhamasisha na kuvutia wawekezaji ikiwemo kwenye sekta ndogo ya saruji. Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Uongozi wa Mkoa wa Kigoma kimeweza kuvutia mwekezaji (Itracom Fertilizers Company Limited) kujenga kiwanda cha saruji na tayari tumeshampa ekari 47 katika Eneo la Uwekezaji la Kigoma (KiSEZ). Wilaya ya Uvinza pia itanufaika na mwekezaji huyu. Serikali inaendelea kuvutia wawekezaji zaidi ili kuwekeza katika Mkoa wa Kigoma ikiwemo Wilaya ya Uvinza. Nakushukuru.