Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 102 2022-09-21

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMISI JUWAKALI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo ya Jeshi kama Chejuu na Dunga, Zanzibar?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA
K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamisi Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum kupitia Kundi la Vijana kutoka Mkoa wa Kusini Unguja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uthamini na upimaji wa maeneo ya Chejuu, na Dunga huko Zanzibar umekamilika, vitabu vya uthamini vipo Kamisheni ya Ardhi Zanzibar. Aidha, kukamilika kwa zoezi hili kunasubiri kukakamilika majadiliano yanayoendelea kati ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Mara majadiliano hayo yatakapokamilika, Wizara itawasilisha maombi ya fedha kwa ajili ya fidia kwa kutumia kiasi cha fedha kilichotengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, aendelee kuwaomba wananchi wa maeneo hayo ya Chejuu, Dunga na maeneo mengine waendelee kuwa na subira wakati tukikamilisha majadiliano hayo. Nakushukuru.