Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 101 2022-09-21

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, ni kwa nini ugonjwa wa TB hauwezi kuonekana kwa mara moja unapompata mwathirika?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ugonjwa wa TB huchelewa kuonekana kutokana na tabia na mwenendo na vimelea vya TB kuzaliana taratibu mwilini na mara nyingi hudhibitiwa na kinga ya mwili wa aliyeambukizwa. Hivyo kila mgonjwa ataanza kuonesha dalili za ugonjwa kutegemea hali ya kinga ya mwili wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa wito kwa wananchi kuwahi mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kupimwa mara tu wanapojisikia dalili zifuatazo; homa za mara kwa mara, kikohozi cha wiki mbili au zaidi, kutoa makohozi yaliyochanganyika na damu, kupungua uzito kwa haraka bila sababu ya msingi na kutokwa jasho jingi hasa usiku. Aidha, ninashauri jamii iwe na utaratibu wa kupima afya mara kwa mara ili kutambua magonjwa mapema na hatimaye kuanza matibabu mapema. Ahsante.