Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 99 2022-09-21

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wenye sifa wa Shehia ya Njuguni, Majenzi na Chomboni – Micheweni wataunganishwa na TASAF?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF iliyoanza rasmi mwezi Januari, 2020 unaendelea katika Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara na Wilaya zote za Zanzibar kwenye vijiji, mitaa na shehia zote ikiwa ni pamoja na zile ambazo hazikufikiwa wakati wa utekelezaji wa kipindi cha kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika shehia ya Njuguni, Kaya 352 ziliandikishwa, Shehia ya Majenzi Kaya 312 ziliandikishwa na Shehia ya Chamboni Kaya 584 ziliandikishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kaya ambazo hazikutambuliwa na kuandikishwa kwa sababu mbalimbali katika kipindi hiki cha pili utaratibu umeandaliwa kwenda kwenye vijiji, mitaa na shehia zote kwa maeneo yote ya utekelezaji ili ziweze kuandikishwa na kuingizwa kwenye mpango ikiwa zimekidhi vigezo na sifa stahiki.