Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 133 2022-09-22

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wananchi wa Kata ya Majengo Tunduma waliovunjiwa nyumba zao?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali namba 133 lililoulizwa na Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kabla sijajibu swali nitoe maelezo machache ya utangulizi. Kikao cha Makatibu Wakuu wa Nchi za Tanzania na Zambia kilichofanyika mwezi Oktoba, 2013, pamoja na mambo mengine kiliazimia kwamba alama za katikati ya mpaka (Intermediate Boundary Pillars) kwa sehemu ya mpaka yenye urefu wa kilomita 50 ziongezwe ili kuzuia ongezeko la shughuli za kibinadamu na pia eneo la hifadhi ya mpaka lipunguzwe kutoka mita 100 kila upande zilizokuwa zinatambulika hapo awali hadi mita 50 kila upande. Hata hivyo, pamoja na maazimio hayo kutekelezwa, baadhi ya wananchi waliendelea kuvamia eneo la hifadhi ya mipaka kwa kujenga makazi.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2017, Serikali ilitoa tamko la kuvunja nyumba zote zilizojengwa katika eneo la hifadhi ya mpaka suala ambalo lilipingwa na wananchi 134 kwa kufungua Shauri Na. 195/2017 katika Mahakama Kuu, Mbeya. Shauri hilo lilifutwa mwaka 2019 na hatimaye jumla ya nyumba 193 zilizokuwa ndani ya eneo la mita 50 za hifadhi ya mpaka zilibomolewa.

Mheshimiwa Spika, kufuatia hatua hiyo, wananchi 35 walifungua tena shauri Na. 12/2019 katika Mahakama Kuu Mbeya kudai fidia kutokana na kubomolewa kwa nyumba zao. Baada ya mazungumzo nje ya Mahakama (mediation) yenye lengo la kuwapatia viwanja mbadala, wananchi hao kushindikana, shauri hilo limepangwa kuendelea kusikilizwa tarehe 5 Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua shauri hilo na kauli yetu ni kwamba tusubiri mwongozo au maamuzi ya mahakama ili tujue hatua zinazofuatia.