Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 20 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 171 2016-05-16

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:-
Vijiji vingi katika Jimbo la Mpanda Vijijini havina huduma ya umeme.
Je, ni lini Serikali itapelekea huduma ya umeme katika vijiji hivyo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Miradi ya REA awamu ya kwanza nay a pili haikuhusisha Jimbo la Mpanda Vijijini. Katika kuhakikisha kwamba wananchi wa Mpanda wanapata umeme wa uhakika Serikali inatarajia sasa kuvipatia umeme vijiji 49 vya Mpanda Vijijini pamoja na Ofisi za Wilaya kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu unaotarajiwa kuanza mwezi Juni, mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Mpanda Vijijini itahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovolt 0.4 yenye urefu wa kilometa 280. Lakini pia ufungaji wa transfoma 64 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 2,452. Gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 9.4.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Uholanzi kupitia Mradi wa ORIO itafunga mitambo mipya ya kuzalisha umeme wa megawatts 2.5 katika Mji wa Mpanda itakayowezesha maeneo mengi kupata umeme wa uhakika. Mradi huu unatarajiwa kuanza mwezi Julai, 2016 na kukamilika mwezi Julai, 2017.