Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 127 2022-09-22

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kituo kipya cha Polisi katika Wilaya ya Chakechake?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, Mbunge Wa Chakechake kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi lina eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi katika Shehia ya Vitongoji lenye ukubwa wa mita za mraba 1,496. Mpango wa Serikali ni kutenga fedha katika bajeti ya mwaka ujao 2023/2024 ili ujenzi uanze. Nashukuru.