Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 126 2022-09-22

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, ni lini Ripoti ya Ukaguzi ya Chama cha Msingi Nanjirinji ‘A’ itatolewa ili hatua zichukuliwe kwa wahujumu wa fedha msimu wa 2021/2022?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ripoti ya Ukaguzi wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Nanjirinji ‘A’ ilikamilika Desemba, 2021 na kuwasilishwa kwenye Mkutano wa wanachama tarehe 23 Mei, 2022. Aidha, ukaguzi ulibaini kuwepo kwa udanganyifu katika nyaraka za mauzo ya ufuta na hivyo kusababisha malipo ya shilingi 93,476,190 kutolipwa kwa wakulima 89 waliouza kilo 39,319 za ufuta.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hali hiyo, Serikali imechukua hatua ya kuvunja Bodi ya Chama hicho na taarifa ya uchunguzi imewasilishwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Lindi kwa ajili ya uchunguzi zaidi na hatua za kisheria kwa waliohusika na ubadhirifu huo.