Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 123 2022-09-22

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -

Je, ni lini vibali vya uwindaji vitatolewa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasli na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uwindaji wa wanyamapori umegawanyika katika makundi mawili ambayo ni uwindaji wa kitalii na uwindaji wa wenyeji/wageni wakazi. Uwindaji wa kitalii ambao unalenga kupata nyara kwa ajili ya watalii unasimamiwa kwa kuzingatia Kanuni za Uwindaji wa Kitalii. Aidha, uwindaji wa wenyeji na wageni wakazi hufanyika kwa ajili ya kitoweo na unasimamiwa kwa kuzingatia Kanuni za Uwindaji wa Wenyeji na Wageni Wakazi.

Mheshimiwa Spika, vibali vya uwindaji wa kitalii vinaendelea kutolewa kwa mujibu wa Kanuni husika ambapo hadi sasa jumla ya minada Saba imefanyika na wadau wamepewa vibali vyao. Kwa upande wa Uwindaji wa wenyeji na wageni wakazi, vibali hivyo vitaanza kutolewa mara baada ya mapitio ya Kanuni za Uwindaji wa Wenyeji na Wageni Wakazi kukamilika.