Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 118 2022-09-22

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: -

Je, kuna mpango wowote kubadili mwelekeo wa ujenzi Barabara ya Tanga kupitia Handeni, Kiberashi, Mrijo, Mondo Bicha hadi Kwamtoro?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kulingana na taarifa ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Tanga, Manyara, Dodoma na Singida utaanzia Handeni - Kibirashi - Kijungu - Kibaya - Goima - Chemba - Donsee – Kwamtoro hadi Kititimo (Singida) ambayo itakuwa na urefu wa kilometa 463.5.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa barabara hii umeanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa kujenga Kilometa 20 kwa sehemu ya Handeni – Mafuleta, ahsante.