Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 151 2022-09-23

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha uwekezaji wa miradi 294 yenye thamani ya dola bilioni 8.04 inatekelezwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Jimbo la Lulindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kuwa uwekezaji wa miradi 294 yenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 8.04 inatekelezwa, Serikali imeendelea kufanya ufuatiliaji na kuhakikisha kuwa mazingira ya uwekezaji nchini yanaendelea kuboreshwa ili kurahisisha utekelezaji na kuvutia mitaji zaidi. Aidha, kuimarisha Kituo cha Huduma ya Mahala pamoja, kutoa huduma za mahala pamoja kwa njia ya kieletroniki lakini pia kuendelea kuwahudumia wawekezaji baada ya kukamilisha uwekezaji. Nakushukuru.