Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 149 2022-09-23

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano katika Kata za Ikoma, Roche, Gobire na Bukura zilizopo mpakani mwa Tanzania na Kenya?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Bukura Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeingia makubaliano na Kampuni ya Simu ya Halotel tarehe 30 Agosti, 2022 kwa ajili ya ujenzi wa mnara katika Kijiji cha Kirongwe kilichopo katika Kata ya Bukura. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, aidha, kwa Kata za Ikoma na Roche zilizopo katika Jimbo la Rorya zimejumlishwa katika kata 763 ambazo zabuni ya kata hizo kwa ajili ya kupeleka huduma za mawasiliano inatarajiwa kutangazwa mapema mwezi Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kata ya Gobiro, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote umepokea changamoto hiyo na kwamba eneo husika litafanyiwa tathimini na litaingizwa kwenye zabuni za miradi ya mawasiliano itakayotangazwa kwa mwaka wa fedha 2023/ 2024.